July 1, 2025

newsline

Timely – Precise – Factual

Sonko Ajiunga na Kinyang’anyiro cha Ugavana Mombasa Kwa Tiketi ya Wiper

Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko amejiunga na kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha ugavana Mombasa.

Wiper Democratic Movement iliwasilisha jina la Sonko kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuwa miongoni mwa walioidhinishwa kushiriki uchaguzi wa mchujo wa chama.

Kalonzo Musyoka leads a section of leaders to visit Mike Sonko in jail |  Pulselive Kenya

Bosi huyo wa zamani wa Kaunti ya Nairobi atachuana vikali na Mbunge wa Kisauni Ali Mbogo, ambaye pia anawania tiketi ya Wiper.

Mshindi atachuana na aliyekuwa Seneta wa Mombasa Hassan Omar, ambaye amepewa tikiti ya moja kwa moja ya UDA.

Mike Sonko Joins Kalonzo Musyoka's Wiper Party after Lengthy Break from  Active Politics - Tuko.co.ke

Tikiti ya ODM ni vita kati ya Mbunge wa Mvita Abdulswamad Sharif Nassir na bilionea wa Mombasa Suleiman Shabal.

Sonko alikaribishwa rasmi kwa Wiper na kiongozi wa chama Kalonzo Musyoka mnamo Machi 25, huku timu yake ikidokeza kwamba anazingatia mipango ya kutwaa tena kiti chake kama mkuu wa Kaunti ya Nairobi.